Monday, July 25, 2016

INTER YATHIBITISHA NAPOLI KUMUWINDA ICARDI.

MKURUGENZI wa michezo wa Inter Milan, Piero Ausilio amethibitisha kuwa wamekuwa mawasiliano na Napoli juu ya Mauro Icardi, wakati akisisitiza mshambuliaji huyo hatakwenda popote. Napoli wameamua kumfukuzia mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentina kama mbadala wa Gonzalo Higuain ikiwa atakwenda Juventus. Hata hivyo, Ausilio amesema Napoli wanapoteza muda wao bure kwani hawana mpango wowote wa hata kuingia katika mazungumzo ya kumuuza nahodha wao huyo. Akiulizwa kuhusiana na suala hilo, Ausilio alikiri kuwepo kwa mawasiliano lakini hawana mpango wowote wa kuwauzia Napoli mshambuliaji huyo.

No comments:

Post a Comment