Monday, July 25, 2016

CHELSEA, EVERTON ZAPIGANA VIKUMBO KUMUWANIA KOULIBALY.

KLABU za Chelsea na Everton zimetajwa kumtaka Kalidou Koulibaly, huku beki huyo akitaka kuondoka Napoli kwa mujibu wa wakala wake. Wiki iliyopita taarifa zilizagaa kuwa beki huyo mwenye umri wa miaka 25 alitolewa ofa ya kwenda Arsenal, ingawa Arsene Wenger alikataa kiasi cha euro milioni 45 kilichohitajika. Everton na Chelsea zimekuwa zikimuwinda Koulibaly kipindi hiki cha usajili na wakala wa nyota huyo wa kimataifa wa Senegal, Bruno Satin amethibitisha mteja wake anaweza kwenda Ligi Kuu. Bruno amesema Jumamosi iliyopita walikutana na kujaribu juu ya kuongezewa mkataba mpya, hata hivyo hawakufikia muafaka kwani madhumuni makubwa ya mchezaji huyo ni kuondoka na sio kuongeza mkataba. Wakala huyo aliendelea kudai kuwa Napoli imekuwa ikisema Koulibaly ni mchezaji mkubwa lakini wamekuwa hawalioni hilo katika ofa yao ya mkataba mpya.

No comments:

Post a Comment