Monday, July 25, 2016

BAADA YA KUACHWA, ARTETA AIFANYIA "UNDAVA" ARSENAL.

KIUNGO wa zamani wa Arsenal, Mikel Arteta amehatarisha kuwaudhi mashabiki wa klabu hiyo kufuatia kufuta vitu vyote katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram ambayo vinahusiana na wakati akiwa Emirates. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania, aliondoka Arsenal mwishoni mwa msimu uliopita kufuatia kumalizika kwa mkataba wake na kuchukua kibarua cha ukocha chini ya Pep Guardiola kwa mahasimu wao wa Ligi Kuu Manchester City. 
Kutokana na kutaka kuanza upya, Arteta alifuta vitu vyote vinavyohusiana na wakati akiwa Arsenal na sasa anafuatilia ukurasa rasmi wa klabu yake hiyo mpya sambamba na wachezaji wengi katika kikosi cha Guardiola. Hata hivyo, Arteta amewaacha baadhi ya marafiki zake wa Arsenal ambao ni Santi Carzola, Hector Bellerin na Petr Cech.

No comments:

Post a Comment