Wednesday, July 27, 2016

JUVENTUS WAKOMAA NA EURO MILIONI 120 KWA POGBA.

KLABU ya Juventus inadaiwa kunga’ang’ania kiasi cha euro milioni 120 kwa ajili ya kiungo Paul Pogba hivyo kuweka uhamisho wake kwenda Manchester United mashakani. Mabingwa hao wa Italia pia wanasisitiza United walipe ada ya wakala Mino Raiola kwa ajili ya dili hilo ambayo ni euro milioni 25 hivyo kumaanisha jumla iwe euro milioni 145 pamoja na mshahara wa euro 300,000 kwa wiki. Taarifa zilizozagaa zinadai kuwa ili usajili huo ukamilike Juventus ndio wanahitaji vitu hivyo jambo ambalo limewafanya United kutulia na kujipanga upya. Mara baada ya kukamilisha usajili wa Gonzalo Higuain jana, ofisa mkuu wa Juventus Beppe Marotta alidokeza kuhusu suala la Pogba akidai kuwa kwasasa kila kitu kimesimama kwanza.

No comments:

Post a Comment