Wednesday, July 27, 2016

IBRAHIMOVIC ABAINISHA KUMCHOMOLEA BECKHAM KWA AJILI YA UNITED.

MSHAMBULIAJI mpya wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic amebainisha kuwa alimkatalia David Beckham na Ligi Kuu ya Marekani-MLS kwa ajili ya kuja kufanya kazi na rafiki yake Jose Mourinho Old Trafford. Nyota huyo wa kimataifa wa Sweden aliondoka Paris saint-Germain-PSG mwishoni mwa msimu uliopita na kupata ofa kadhaa kabla ya kuamua kujiuanga na United na kucheza kwa mara ya kwanza katika Ligi Kuu. Beckham akiwa tayari ameshanunua ardhi kwa ajili ya ujenzi wa uwanja mpya jijini Miami, nahodha huyo wa zamani wa Uingereza alijaribu kumshawishi mchezaji mwenzake huyo wa zamani wa PSG kujiunga naye wakati klabu yake ikiw ana lengo la kuingia MLS mwaka 2018. Akihojiwa Ibrahimovic amesema Beckham ni rafiki yake mkubwa na alimuambia aende kucheza katika timu yake ya Miami lakini alimkatalia kwasababu anaamini wakati huu haukuwa muafaka. Nyota huyo amesema kwasasa anataka kufanya vitu vikubwa akiwa na United, labda pengine huko mbele ndio anaweza kufikiria kwenda MLS.

No comments:

Post a Comment