Wednesday, July 27, 2016

ARSENAL MAJANGA.

BEKI wa Arsenal, Per Mertesacker anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa miezi kadhaa kufuatia kusumbuliwa na majeruhi ya goti yaliyomzuia kujiunga na wachezaji wenzake katika ziara ya Amerika Kaskazini. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger alinainisha hayo katika mkutano wake na wanahabari kuelekea mchezo wao wa kirafiki dhidi ya nyota wa Ligi Kuu ya Marekani-MLS utakaofanyika huko San Jose. Wenger amesema Mertesacker alipata majeruhi hayo katika mchezo wao wa kirafiki dhidi ya Lens Ijumaa iliyopita na sasa inabidi watafute mbadala ili wapate mchezaji mwenye uzoefu katika nafasi hiyo. Meneja huyo pia alithibitisha kuwa mchezaji mpya aliyesajiliwa msimu huu Granit Xhaka naye atapata nafasi ya kucheza katika mchezo huo.

No comments:

Post a Comment