Wednesday, July 27, 2016

GUARDIOLA APIGA CHINI VIBONGE CITY.

MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola amewaengua mazoezini baadhi ya wachezaji wake katika kikosi cha kwanza mpaka hapo watakapofikia uzito unaohitajika. Beki wa timu hiyo, Gael Clichy amesema meneja huyo raia wa Uholanzi amewataka wachezaji kuepuka kula pizza, juice na vyakula vingine vizito ili kuepuka kuongezeka uzito. Akihojiwa kuhusiana na hilo, Guardiola amesema sio kwamba wachezaji hao wamezidi uzito lakini anataka wachezaji wake wawe fiti. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa suala la uzito ni muhimu kwani mchezaji anapokuwa hayupo fiti kuna athari kadhaa ikiwemo kushindwa kuwa kasi ya kutosha au kushindwa kuruka juu kwa haraka. City wanatarajiwa kukwaana na Borussia Dortmund kesho katika mchezo wa kirafiki wa michuano ya Kimataifa utakaofanyika huko Shenzhen, China.

No comments:

Post a Comment