Wednesday, July 27, 2016

HIGUAIN APEWA NAMBA 9 JUVENTUS.

MSHAMBULIAJI mpya wa Juventus, Gonzalo Higuain amepewa jezi namba 9 kwa ajili ya kampeni za msimu 2016-2017. Higuain ambaye amejiunga na mabingwa hao wa Serie A kwa kitita cha euro milioni 90 na kuwa mchezaji wa tatu kusajiliwa kwa fedha nyingi katika historia ya soka, alitambulishwa mbele ya mashabiki baada ya kukamilisha vipimo vya afya. Mashabiki wa Juventus walimpokea kwa shangwe shujaa wao huyo mpya ambaye ametua Turin akitokea kwa mahasimu wao Napoli. Jezi namba tisa imekuwa ikivaliwa na nyota kadhaa waliowahi kupita katika klabu hiyo akiwemo Alvaro Morata, Zlatan Ibrahimovic na Marcelo Salas.

No comments:

Post a Comment