Wednesday, July 27, 2016

MASCHERANO AKUBALI KUBAKI BARCELONA.

KLABU ya Barcelona imetangaza kufikia makubaliano na Javier Mascherano juu ya mkataba mpya na ulioboreshwa wa miaka mitatu. Nyota huyo wa kimataifa wa Juventus amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda Juventus ambao tayari wameshamsajili Dani Alves mapema kiangazi hiki. Hata hivyo, mkurugenzi wa taasisi ya mahusiano Albert Soler amethibitisha kuwa Mascherano amekubalia kubakia katika klabu hiyo aliyojiunga nayo mwaka 2010 akitokea Liverpool. Soler amesema kwasasa hawawezi kuzungumzia tena kuhusu Mascherano kwani tayari ameshakubali kuongeza miaka mingine mitatu. Taarifa hizo zimetoka wakati Barcelona wakimtambulisha kiungo wao mpya Andre Gomes ambaye wamemsajili kutoka Valencia kwa mkataba wa miaka mitano.

No comments:

Post a Comment