Wednesday, July 27, 2016

KLABU KUFANYA MABADILIKO WACHEZAJI WANNE KATIKA FA MSIMU HUU.

KLABU zitaruhusiwa kutumia mchezaji wanne wa akiba wakati wa muda wa nyongeza katika hatua za mwishoni za michuano ya Kombe la FA msimu huu. Mfumo huo ambao unatarajiwa kupitishwa na Bodi ya Kimataifa ya Soka ulifanyiwa majaribio katika michuano ya Copa America kiangazi hiki. Sheria hiyo inatarajiwa kuanza kutumika katika Kombe la FA kuanzia hatua ya robo fainali. Ofisa mkuu wa Chama cha Soka cha Uingereza-FA, Martin Glenn amesema hatua hiyo ni muhimu na ajili ya manufaa ya wachezaji. Michuano ya mwaka huu ya FA inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Ijumaa ya Agosti 5 wakati mechi 184 za hatua ya awali zitafanyika.

No comments:

Post a Comment