Friday, July 29, 2016

KAZI ZA UN ZILINIPA UZOEFU WA KUFANYA KAZI FIFA - SAMOURA.

KATIBU mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Fatma Samoura amesema miaka aliyotumia kufanya kazi katika kingo za vita wakati akiwa Umoja wa Mataifa ndio uliomuandaa kuja kufanya kazi yake hiyi mpya. Mwanamama huyo raia wa Senegal mwenye umri wa miaka 54, alianza rasmi kibarua chake katika shirikisho hilo mwezi uliopita. Akihojiwa Samoura amesema amefanya kazi karibu maeneo yote ya hatari duniani ikiwemo Afghanistan, Liberia, Sierra Leone, Timor ya Mashariki, Kosovo na Nigeria. Samoura aliendelea kudai kuwa anadhani miaka yake 20 iliyopita katika shughuli ilimuandaa vyema tayari kwa kibarua hicho. Samoura anakuwa mwanamke wa kwanza kushikilia wadhifa wa Katibu Mkuu wa FIFA toka kuanzishwa kwake.

No comments:

Post a Comment