Friday, July 29, 2016

GUARDIOLA AELEZA UCHU WAKE KWA STONES.

MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola amethibitisha kuwa na nia ya kumsajili beki wa Everton John Stones. Inadaiwa kuwa Everton wanataka kiasi cha paundi milioni 50 kwa ajili ya beki huyo mwenye umri wa miaka 22 ambaye kiangazi mwaka jana alikaribia kiduchu kujiunga na Chelsea. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo mara baada ya mchezo wao wa kirafiki dhidi ya Borussia Dortmund ambao walishinda kwa changamoto ya mikwaju penati 6-5, Guardiola amesema kila mtu anafahamu kuwa watajaribu kumsajili. Stones alikuwa sehemu ya kikosi cha Uingereza kilichokwenda kushiriki michuano ya Ulaya mwaka huu lakini hakucheza mechi yeyote wakati nchi hiyo ilipotolewa katika hatua ya timu 16 bora.

No comments:

Post a Comment