Friday, July 29, 2016

MSHINDI WA PUSKAS AWARD ATUNDIKA DARUGA.

MSHAMBULIAJI wa Brazil, Wendell Lira ameacha kucheza mpira miezi sita baada ya kushinda tuzo ya bao bora la mwaka inayojulikana kama Puskas Award, ili aweze kuanza kazi yake mpya ya kuwa mchezaji wa mipira ya kwenye video. Bao alilofunga nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 kwa timu yake ya Goianesia dhidi ya Atletico Goianiense ndio lililompatia tuzo hiyo na kuwapiku nyota wengine kama Lionel Messi na Alessandro Florenzi katika tuzo za Ballon d’Or Januari mwaka huu. Lakini nyota huyo sasa ametangaza kutundika daruga zake na kuamua kujikita zaidi katika shughuli za michezo ya video. Moja ya sababu kubwa zilizomfanya kuachana na soka amesema ni uongo uliokithiri huku akishindwa kufafanua zaidi kwa undani suala hilo.

No comments:

Post a Comment