Thursday, July 21, 2016

MAN UNITED YAKUBALI KUMWAGA EURO MILIONI 110 KWA POGBA.

KLABU ya Manchester United inadaiwa kukubali kuvunja rekodi ya uhamisho kwa kumsajili Paul Pogba kwa kitita cha euro milioni 110. Maofisa wa klabu hiyo ya Ligi Kuu walikutana na maofisa wa Juventus mapema jana kujadili uhamisho wa kumpeleka Pogba Old Trafford. Sasa imefahamika kuwa United wamekubali kutoa kitita cha euro milioni 110 kwa Pogba ambacho kitapita kile kiwango kilichovunja rekodi wakati Real Madrid walipolipa euro milioni 100 kwa ajili ya gareth Bale mwaka 2013. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka mitano Old Trafford. Kiungo anadaiwa kuwa tayari kukubali mshahara wa euro milioni 13 kwa mwaka akiwa Old Trafford, kiwango ambacho kitakuwa ni karibu mara tatu ya mshahara anaochukua hivi sasa Juventus.

No comments:

Post a Comment