Friday, July 29, 2016

SCHWEINSTEIGER ATUNDIKA DARUGA SOKA LA KIMATAIFA.

NAHODHA wa timu ya taifa ya Ujerumani, Bastian Schweinsteiger ametangaza kustaafu rasmi soka la kimataifa. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 31 anayekipiga katika klabu ya Manchester United, alikuwa sehemu ya kikosi cha Ujerumani kilichotwaa Kombe la Dunia nchini Brazil mwaka 2014. Schweinsteiger anastaafu akiwa mchezaji wan ne kuitumikia nchi yake mechi nyingi zaidi, akiwa amecheza mechi 120 nyuma ya Lothar Matthaus aliyecheza mechi 150, Miroslav Klose mechi 137 na Lukas Podolski mechi 129. Nyota huyo aliitwa kwa mara ya kwanza katika kikosi cha Ujerumani mwaka 2004 na anashikilia rekodi ya kuichezea nchi hiyo mechi nyingi zaidi za michuano ya Ulaya, akiwa amecheza mechi 15.

No comments:

Post a Comment