Friday, July 29, 2016

KLOPP AMPONDA MOURINHO "KIAINA"

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp amekiri kuwa hatishiki na klabu mahasimu ambao wanasajili wachezaji kwa fedha nyingi na kudai kuwa yeye anataka kufanya mambo tofauti Merseyside. Kutokana na Manchester United chini ya Jose Mourinho kukaribia kufanya usajili wa kiungo wa Juventus Paul Pogba kwa zaidi ya paundi milioni 100, meneja huyo wa zamani wa Borussia Dortmund anafurahia mipango yao ya usajili. Liverpool imesajili wachezaji wawili kwa fedha nyingi kiaangazi hiki ambao ni Saido Mane waliyemsajili kutoka Southampton kwa kiasi cha paundi milioni 34 na kiungo wa Newcastle United Georgio Wijnaldum aliyesajili kwa paundi milioni 23. Akihojiwa Klopp amesema kama unasajili mchezaji mmoja kwa paundi milioni 100 halafu anakuja kuumia mambo yote lazima yaende vibaya ndio maana hataki kutumia fedha nyingi kwa ajili ya mchezaji mmoja.

No comments:

Post a Comment