Friday, July 29, 2016

SHABIKI AKAMATWA CHUMBA CHA KUFULIA HOTELINI AKITAKA KUONANA NA NEYMAR.

SHABIKI wa nyota wa Barcelona, Neymar amekamatwa baada ya kukutwa katika chumba cha kufulia katika hoteli waliyofikia timu ya taifa ya Brazil kuelekea katika michuano ya Olimpiki itakayofanyika jijini Rio de Janeiro. Neymar na wachezaji wenzake kwasasa wanajiandaa na michuano hiyo inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi mwezi ujao ambapo wataanza kwa kucheza na Afrika Kusini Agosti 4 na pia kucheza na Iraq na Denmark katika mechi zao zingine za kundi A. Maandalizi yao yaliathiriwa kwa muda na kijana mwenye umri wa miaka 21 aliyefanikiwa kupenya na kuingia katika hoteli hiyo iliyopo katika mji wa Goiania. Ofisa wa polisi Vladimir Passos aliwaambia wanahabari kuwa wafanyakazi wa hoteli waligundua kitu tofauti na kuwaita kuja kumkamata kijana huyo ambaye alijitetea kuwa alikuwa akitaka kuonana na Neymar. Hata hivyo, inadaiwa kuwa baadae kijana huyo alihojiwa baada ya kuhojiwa na kugundulika alitumia kitambulisho feki cha Shirikisho la Soka la Brazil-CBF kilichomuwezesha kuingia hotelini humo.

No comments:

Post a Comment