Tuesday, August 30, 2016

BARCELONA YAANZA MAZUNGUMZO YA MKATABA MPYA NA MESSI.

RAIS wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu amesema mazungumzo yameshaanza kwa ajili ya Lionel Messi kusaini mkataba mpya. Messi yuko chini ya mkataba mpaka mwaka 2018 lakini Barcelona wanataka kumpa ofa ya mkataba mpya kufuatia taarifa kuzagaa Julai mwaka huu kuwa walishakubaliana dili jipya. Akihojiwa kuhusiana na hilo, Bartomeu amesema Messi bado ana miaka miwili katika mkataba wake lakini watazungumza naye kwa ajili ya kumuongeza kwasababu wanataka kuendelea kuwa naye. Kwasasa Messi anasumbuliwa na majeruhi ya msuli wa paja wakati Argentina ikijiandaa kukwaana na Uruguay na Venezuela katika mechi za kufuzu Kombe la Dunia.

No comments:

Post a Comment