Tuesday, August 30, 2016

HART KWENDA TORINO KWA MKOPO.

WAKALA wa Joe Hart amethibitisha kuwa mteja wake anatarajiwa kujiunga na klabu ya Torino ya Italia wakati akikaribia kuondoka Manchester City. Hart anaondoka City kufuatia kutomvutia meneja mpya Pep Guardiola ambaye tayari ameshamnunua Claudio Bravo kutoka Barcelona ili kuziba nafasi yake. Kipa huyo wa kimataifa wa Uingereza alicheza mechi yake ya mwisho na City katika mchezo wa kufuzu hatua ya makundi dhidi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Steaua Bucharest ya Romania. Akihojiwa kuhusiana na hilo wakala wa Hart, Jonathan Barnett alithibitisha kuwa mteja wake huyo amekubali kujiunga na Torino kwa mkopo wa msimu mzima. Barnett aliendelea kudai kuwa tayari City nao wameshatoa ruksa na sasa kinachosubiriwa ni vipimo vya afya kabla ya kukamilisha dili hilo.

No comments:

Post a Comment