Friday, August 26, 2016

BARCELONA YAMKAZIA ALCACER.

KLABU ya Barcelona inadaiwa kukubali kuongeza ofa kwa ajili ya mshambuliaji wa Valencia Paco Alcacer mpaka kufikia euro milioni 30 baada ya kumuuza Claudio Bravo. Mabingwa hao wa Hispania wamefanikiwa kupata faida ya euro milioni tano kwa kumuuza Bravo Manchester City na kumleta kipa wa Ajax Amsterdam Jasper Cillessen kuja kuziba pengo lake. Huku wakiwa wamebaki na euro milioni 24 katika bajeti yao ya usajili, Barcelona sasa wako katika nafasi nzuri ya kufikia ada inayohitajika kwa ajili ya mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 24. Deportivo inadaiwa kuwa itakubali kiasi cha kuanzia euro milioni 30 na 35 kwa ajili kumuachia Alcacer kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili Jumatano ijayo.

No comments:

Post a Comment