Friday, August 26, 2016

WEST HAM YSAJILI NYOTA KUTOKA USWISI.

KLABU ya West Ham United imetangaza kumsajili kiungo wa kimataifa wa Uswisi, Edimilson Fernandes. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 20 anejiunga na klabu hiyo ya Ligi Kuu akitokea FC Sion kwa mkataba wa miaka minne. Fernadez amefunga mabao sita katika mechi 66 alizoichezea mabingwa hao wa mara mbili wa Uswisi. Akihojiwa mara baada ya kusaini mkataba huo, Fernandez amesema kutua West Ham ni changamoto mpua kwake na sasa jukumu limebaki kwake kuhakikisha anafanya bidii ili kuja kuwa mchezaji mkubwa.

No comments:

Post a Comment