Friday, August 26, 2016

ARSENAL YAKARIBIA KUWANASA PEREZ NA MUSTAFI.

KLABU ya Arsenal, inadaiwa kukubali dili la kuwasajili mshambuliaji wa Deportivo La Coruna Lucas Perez na beki wa Valencia Shkodran Mustafi na wote wanatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya muda wowote kuanzia sasa. Maofisa wa Arsenal wamekuwa wakiumiza vichwa katika kipindi hiki cha usajili wa kiangazi kutokana na majeruhi waliyonayo katika safu ya ulinzi na kutokuwa na washambuliaji wa kutosha na hatimaye wamefikia makubaliano ya kuleta nyota wawili kutoka La Liga. Perez mwenye umri wa miaka 27, amefunga mabao 17 katika ligi msimu uliopita na amekuwa akifuatiliwa mara kadhaa na maskauti wa Arsenal ambao baadae waliamua kumtolea ofa Jamie Vardy. Hata hivyo, mshambuliaji huyo wa Leicester City alikataa uhamisho wa kwenda Emirates kwa kusaini mkataba mpya na klabu hiyo na kuacha Arsene Wenger akitafuta washambuliaji wengine. Jana usiku Deportivo walithibitisha kuwa Perez amepewa ruhusa ya kukosa mchezo wa Ijumaa wa La Liga dhidi ya Real Betis.

No comments:

Post a Comment