Friday, August 26, 2016

RANIERI AJIPA MOYO.

MENEJA wa Leicester City, Claudio Ranieri ana uhakika haitachukua muda mrefu kabla ya kikosi chake hakijarejesha makali yao yaliyowafanya kutwaa ubingwa wa Ligi kuu msimu uliopita. Leicester walianza vibaya msimu kwa kufungwa na Hull City waliopanda daraja msimu huu kabla ya kuja kutoa sare ya bila kufunga na Arsenal. Akihojiwa Ranieri amesema anadhani wachezaji wapya waliowasajili hatachukua muda mrefu kabla ya kuzoeana na wenzao. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa ana matumaini kikosi chake kitapata matokeo mazuri katika mchezo wao dhidi ya Swansea City kesho.

No comments:

Post a Comment