Friday, August 26, 2016

UEFA YAFANYA MABADILIKO CHAMPIONS LEAGUE NA EUROPA LEAGUE.

SHIRIKISHO la Soka la Ulaya-UEFA limefanya mabadiliko kidogo katika michuano yao wanayoandaa kuanzia msimu wa 2018-2019. Mabadiliko hayo yaliyofanywa ni kuruhusu ligi nne bora barani Ulaya kupata nafasi nne za moja kwa moja katika hatua za makundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Ligi hizo nne kwa mujibu wa viwango vya UEFA ni Hispania, Ujerumani, Uingereza na Italia. Chini ya mfumo wa sasa, Uingereza, Ujerumani na Hispania zote zina nafasi tatu za kufuzu moja kwa moja kasoro ile ya nne ambayo lazima igombaniwe ili kufuzu. Italia wao wana nafasi mbili pekee za kufuzu moja kwa moja katika hatua ya makundi huku moja ya tatu ikiingia katika mzunguko wa mtoano. UEFA pia imedai kuwa timu zinazofuzu nafasi ya kushiriki michuano ya Europa League nazo pia zitafuzu moja kwa moja hatua ya makundi katika mfumo huo mpya.

No comments:

Post a Comment