Friday, August 26, 2016

THIERRY HENRY ALAMBA SHAVU UBELGIJI.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa na klabu za Arsenal na Barcelona Thierry Henry ameteuliwa kuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Ubelgiji. Henry anajiunga katika benchi la ufundi la timu hiyo linaloongozwa na Roberto Martinez ambaye alichukua nafasi ya Marc Wilmots mwanzoni mwa mwezi huu. Martinez ambaye ni meneja wa zamani wa Everton, amesema Henry ni mtu muhimu na ataleta kitu tofauti katika kikosi hicho. Henry mwenye umri wa miaka 39, anatarajiwa kufanya kazi sambamba na Graeme Jones ambaye amekuwa akifanya kazi na Martinez katika klabu za Swansea City, Wigan Athletic na Everton.

No comments:

Post a Comment