Tuesday, August 30, 2016

DEAL DONE: MUSTAFI NA PEREZ.

KLABU ya Arsenal imekamilisha rasmi usajili wake wa wachezaji wawili kwa mpigo ambao umewagharimu zaidi ya paundi milioni 50. Nyota hao wawili waliosajiliwa ni mshambuliaji wa Deportivo La Coruna Lucas Perez na beki wa Valencia Shkodran Mustafi. Perez mwenye umri wa miaka 27 amesajiliwa kwa kitita cha paundi milioni 17.1 huku Mustafi yeye akisajiliwa kwa paundi milioni 35. Arsenal sasa inakuwa imesajili wachezaji sita kiangazi hiki bada ya Granit Xhaka na chipukizi Rob Holding, Takuma Asano na Kelechi Nwakali. Akimzungumzia Perez, meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesema mshambuliaji huyo sio kwamba anaweza kufunga mabao pekee bali pia anaweza kucheza vyema na wenzake. Kwa upande wa Mustafi Wenger amesema yuko katika umri sahihi na ana uzoefu mzuri pamoja na utulivu mkubwa pindi anapokuwa na mpira.

No comments:

Post a Comment