Wednesday, August 31, 2016

BENTEKE AMKUMBUKA RODGERS.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Ubelgiji, Christian Benteke amesisitiza kuwa hakushindwa Liverpool, lakini anadhani muda wake ungekuwa na mafanikio zaidi kama klabu hiyo isingemtimua Brendan Rodgers. Benteke alinunuliwa kwa kitita cha pauni milioni 32.5 akitokea Aston Villa Julai mwaka 2015 wakati huo Liverpool ikiwa chini ya Brendan Rodgers. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 25, alianza katika mechi sita za kwanza za ligi kabla ya Rodgers hajatimuliwa Octoba na nafasi yake kuchukuliwa na Jurgen Klopp. Kufuatia ujio wa meneja huyo mpya, Benteke hakufanikiwa kupata nafasi na badala yake Mjerumani huyo alipendelea kuwatumia zaidi Firmino na Divock Origi. Akihojiwa kufuatia uhamisho wake kwenda Crystal Palace uliogharimu kiasi cha pauni milioni 32, Benteke anaamini hakufanikiwa kufanya vizuri Liverpool lakini anadhani angefanya vyema zaidi kama angepewa nafasi ya kucheza.

No comments:

Post a Comment