Wednesday, August 31, 2016

GUARDIOLA ADAI HAKUNA TIMU INAYOFIKIA KIWANGO CHA BARCELONA.

MENEJA wa Manchester City Pep Guardiola amemmwagia sifa Luis Enrique na Barcelona, akisisitiza hakuna yeyote katika ulimwengu wa soka anayecheza vizuri zaidi ya mabingwa hao wa La Liga kuelekea mchezo baina yao. Guardiola atapambana na klabu yake hiyo ya zamani baada ya City kupangwa kundi moja na Barcelona katika hatua ya makundi ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Hiyo itakuwa mara ya tatu na nne kwa Guardiola kukutana na Barcelona toka alipoondoka mwishoni mwa msimu wa 2011-2012. Mara ya mwisho alikutana nao akiwa meneja wa Bayern Munich katika nusu fainali ya michuano hiyo misimu miwili iliyopita ambapo aliondoshwa kwa jumla ya mabao 5-3. Akihojiwa kuhusiana na hilo, Guardiola amesema kwa mara nyingine kucheza na Barcelona itakuwa jaribio gumu kwake haswa kutokana na safu imara ya ushambuliaji waliyonayo ambayo inaongozwa nyota watatu Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar.

No comments:

Post a Comment