Wednesday, August 31, 2016

ARSENAL WAPAISHA USAJILI WA LIGI KUU KUFIKIA ZAIDI PAUNDI BILIONI MOJA.

KLABU za Ligi Kuu sasa zimetumia zaidi ya pauni bilioni moja katika usajili wao waliofanya kipindi hiki cha kiangazi. Ligi hiyo ilikuwa tayari imeshavunja rekodi yake yenyewe ya usajili wiki iliyopita, wakati Manchester City walipomsajili kipa wa Barcelona Claudio Bravo na kupelekea kufikia kiasi cha paundi milioni 880 wakizidi paundi milioni 870 zilizotumika kiangazi mwaka jana. Arsenal kukamilisha usajili wa beki wa kimataifa wa Ujerumani Shkodran Mustafi kutoka Valencia aliyenunuliwa kwa ada ya pauni milioni 35 jana usiku kunapelekea jumla ya fedha zilizotumika katika usajili mpaka sasa kufikia zaidi ya paundi bilioni moja huku zikibaki saa chache kabla ya dirisha kufungwa leo usiku. Huu unakuwa msimu wa nne wa majira ya kiangazi kwa rekodi mpya kuwekwa katika usajili wa Ligi Kuu. Hull City imekuwa klabu ya 12 kuvunja rekodi yao ya usajili kiangazi hiki wakati walipomnyakuwa Ryan Mason kutoka Tottenham Hotspurs.

No comments:

Post a Comment