Wednesday, August 31, 2016

CHELSEA YAMUWANIA TENA DAVID LUIZ.

KLABU ya Chelsea inadaiwa kuingia katika mzungumzo ya kumuwania David Luiz kutoka Paris Saint-Germain kwa kitita cha paundi milioni 32. Chelsea wamekuwa katika mazungumzo na Kia Joorabchian na Giuliano Bertolucci toka waliposhindwa kumsajili Kalidou Koulibaly kutoka Napoli. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 amesema yuko tayari kuondoka na alicheza kwa mafanikio wakati aliposajiliwa kwa mara ya kwanza Chelsea akitokea Benfica kwa kitita cha paundi milioni 21 Januari mwaka 2011. Hata hivyo, uhamisho huo utawezekana pale tu, PSG watakapofanikiwa kupata mbadala wa beki huyo.

No comments:

Post a Comment