Wednesday, August 31, 2016

BONY KWENDA STOKE.

KLABU ya Stoke City inadaiwa kukaribia kumsajili mshambuliaji wa Manchester City Wilfried Bony. Bony aliwasili katika uwanja wa mazoezi wa Stoke mapema leo ikiwa ni mchakato wa kukamilisha uhamisho wake kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili, ingawa klabu hizo mbili zinadaiwa bado kufikia muafaka wa mwisho. Nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast bado hajacheza katika mechi yeyote msimu huu na City wamekuwa wakimtafutia klabu mpya katika wiki za karibuni. West Ham United, pamoja na kumnunua Simone Zaza mwishoni mwa wiki iliyopita nao walikuwa wakitajwa kumuwania Bony mpaka jana usiku lakini sasa wanaonekana kujitoa kwenye kinyang’anyiro hicho. Bony mwenye umri wa miaka 27 ni mmoja kati ya wachezaji wa kikosi cha kwanza ambao wanategemewa kuondoka kabla ya dirisha la usajili kufungwa leo usiku, wengine ni Samir Nasri, Joe hart na Eliaquim Mangala.

No comments:

Post a Comment