Wednesday, August 31, 2016

WILSHERE KWENDA PALACE AU BOURNEMOUTH.

KIUNGO wa Arsenal, Jack Wilshere anatarajiwa kujiunga na Crystal Palace au Bournemouth kwa mkopo wa msimu mzima ili aweze kupata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 amekutana na meneja wa Palace, Alan Pardew na yule wa Bournemouth Eddie Howe jana kwa ajili ya mazungumzo. Wilshere ameichezea Uingereza mechi sita katika kipindi cha kiangazi zikiwemo mechi tatu za michuano ya Ulaya lakini ameachwa katika kikosi cha nchi hiyo kinachoongozwa na kocha mpya Sam Allardyce. Kutokana na Wilshere kuandamwa na majeruhi ya mara kwa mara, Arsenal waliamua kumnunua kiungo wa kimataifa wa Uswisi Granit Xhaka kwa kitita cha pauni milioni 35 kiangazi hiki.

No comments:

Post a Comment