Thursday, August 25, 2016

DRINKWATER NAYE AFUATA NYAYO ZA KINA VARDY LEICESTER.

KIUNGO wa Leicester City, Danny Drinkwater amesaini mkataba mpya wa miaka mitano na mabingwa hao wa Ligi Kuu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26, alikuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha timu hiyo ambacho kiliushangaza ulimwengu chini ya meneja Claudio Ranieri kwa kutwaa ubingwa msimu uliopita. Akihojiwa mara baada ya kusaini mkataba huo utakaomalizika mwaka 2021, Drinkwater amesema anafuraha kubwa kwani anapenda kuitumikia timu hiyo na anaona ndio pekee inayomfaa kwasasa. Drinkwater anafuata nyayo za nyota wenzake wa timu hiy ambao wameongeza mikataba yao kiangazi hiki akiwemo Jamie vardy, Riyad Mahrez, Wes Morgan, Kasper Scheichel na Andy king.

No comments:

Post a Comment