Monday, August 29, 2016

SCHURRLE AACHWA KIKOSI CHA UJERUMANI.

WINGA wa Borussia Dortmund, Andre Schurrle amelazimika kuondolewa katika kikosi cha Ujerumani kwa ajili ya mechi ya kimataifa ya kirafiki na kufuzu Kombe la Dunia kutokana na majeruhi. Schurrle alilalamika kuzumbuliwa na maumivu ya mgongo kufuatia ushindi wa mabao 2-1 waliopata Dortmund dhidi ya Mainz katika mchezo wao wa ufunguzi wa Bundesliga jana. Majeruhi hayo yanamaanisha kuwa Schurrle hatakuwepo katika mchezo wa kirafiki wa Ujerumani dhidi ya Finland ambao utafanyika huko Monchengladbach au ule wa kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Norway Septemba 4. Taarifa kutoka Shirikisho la Soka la Ujerumani lilithibitisha taarifa hizo na kuongoza haijajulikana kama kocha Joachim Low ataamua kuita mchezaji mwingine ili kuziba nafasi yake. Katika mechi za kufuzu Kombe la Dunia litakalofanyika nchini Urusi, Ujerumani wamepangwa kundi C sambamba na Norway, Ireland Kaskazini, Jamhuri ya Czech, Azerbaijan na San Marino.

No comments:

Post a Comment