Monday, August 29, 2016

WENGER AMFANANISHA XHAKA NA EMMANUEL PETIT.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amepongeza ujio wa Granit Xhaka katika kikosi chake na kumfananisha na kiungo wa zamani wa timu hiyo Emmanuel Petit. Xhaka aliyesajiliwa kiangazi hiki alianza katika mechi zote dhidi ya Leicester City na Watford, huku kiwango chake kikiboreka zaidi katika mchezo wa juzi huko Vicarage Road. Wenger anaamini nyota huyo wa kimataifa wa Uswisi ana kila kitu ambacho kinafanana na Petit aliyetwaa taji la Ligi Kuu akiwa na Arsenal katika msimu wa 1997-1998. Akihojiwa Wenger amesema Xhaka huwa anakuwa mtulivu pindi awapo na mpira na kwa mbali anafanana na Petit ka aina ya soka lake.

No comments:

Post a Comment