Saturday, September 24, 2016

BABA YAKE YAYA TOURE AMUOMBEA MSAMAHA MWANAYE KWA GUARDIOLA.

BABA wa kiungo wa Manchester City Yaya Toure amemtaka meneja wa klabu hiyo Pep Guardiola kujishusha na kumpa mwanaye nafasi nyingine. Mapema wiki hii Guardiola amesema hatampanga Toure katika kikosi chake tena mpaka pale wakala wake Dimitri Seluk atakapokuja kumuomba radhi kwa kauli aliyotoa katika vyombo vya habari. Mzee huyo aitwaye Mory amesema ana wasiwasi kwani kuna tatizo na anamuomba Guardiola kusamehe na kumruhusu mwanaye kufanya kazi yake. Pamoja na Guardiola kutaka kuombwa radhi na Seluk, wakala huyo alijibu mapigo na kumtuhumu meneja huyo anajidai kuwa kashinda kila kitu hivyo anaweza kufanya chochote anachotaka.

No comments:

Post a Comment