Monday, September 26, 2016

DE BRUYNE KUKAA NJE WIKI NNE.

KIUNGO wa Manchester City Kevin De Bruyne anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa kipindi cha wiki nne kufuatia majeruhi ya msuli wa paja aliyopata katika ushindi wa Jumamosi dhidi ya Swansea City. De Bruyne alitolea kufuatia kupata majeruhi hayo katika dakika ya 81 ya mchezo ambao City ilishinda mabao 3-1 na sasa taarifa zinadai kuwa atakaa nje kwa kipindi cha mwezi mmoja. Hatua hiyo sasa inamaanisha De Bruyne atakosa mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Celtic Jumatano hiipamoja na mechi mbili za Ligi Kuu dhidi ya Tottenham Hotspurs na Everton wakati pia kukiwa na hatihati ya kukosa safari ya kuifuata Barcelona Octoba 19 mwaka huu. Nyota huyo pia atakosa mechi za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia za Ubelgiji ambao watacheza dhidi ya Bosnia-Herzegovina na Gibraltar.

No comments:

Post a Comment