Monday, September 26, 2016

TP MAZEMBE, MO BEJAIA KUVAANA FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO.

KLABU ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC inatarajiwa kukwaana na Mouloudia Bejaia ya Algeria katika fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho. Timu hizo zote mbili zimepata nafasi ya kutinga hatua hiyo kwa sheria ya bao la ugenini ambapo Mazembe wao walitoka sare ya bila ya kufungana na Etoile de Sahel ya Tunisia jana jijini Lubumbashi na kusonga mbele kwa sare ya bao 1-1 waliyopata ugenini katika mchezo wao wa mkondo wa kwanza. Kwa upande wa Mo Bejaia wao walisonga mbele baada ya kupata sare ya bao 1-1 ugenini dhidi ya FUS Rabat ya Morocco kufuatia timu hizo kutoka sare ya bila kufungana katika mchezo wao wa kwanza. Fainali ya michuano hiyo ambayo itapigwa kwa mikondo miwili inatarajiwa kufanyika Octoba na Novemba mwaka huu.

No comments:

Post a Comment