Wednesday, September 28, 2016

KIPA WA MAURITIUS ADAKWA NA DAWA ZA KULEVYA.

GOLIKIPA wa kimataifa wa Mauritius, Joseph Kinsley Steward Leopold amekamatwa kwa tuhuma za kushughulika na madawa ya kulevya. Kikosi kazi cha kupambana na dawa hizo nchini humo, kilikwenda kupekua nyuma ya kipa huyo mwenye umri wa miaka 27 iliyopo huko Port Louis na kukuta pakiti 22 za dawa aina ya heroin. Vifaa vingine vinavyotumika kuandaa na kuhifadhi heroin vikiwemo viwembe na mizani pia vilikutwa katika nyumba ya kipa huyo. Leopold ni kipa chaguo la kwanza la timu ya ASPL 2000 inayoshiriki Ligi Kuu ya nchi hiyo na pia alikuwa kipa wa akiba wa timu ya taifa katika mechi ya mwisho ya kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika.

No comments:

Post a Comment