Thursday, September 22, 2016

MESSI NJE WIKI TATU.


MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Lionel Messi anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa muda wa wiki tatu baada ya kupata majeruhi ya nyonga katika sare ya bao 1-1 waliyopata dhidi ya Atletico Madrid. Nyota huyo alitolewa katika dakika ya 59 ya mchezo huo baada ya kukwatuliwa na Diego Godin. Messi alilazimika kukosa mchezo wa Argentina wa kufuzu michuano ya Kombe la Dunia 2018 dhidi ya Venezuela mapema mwezi huu kutokana na matatizo kama hayo lakini amefanikiwa kucheza mechi zote za La Liga msimu huu. Kama hali ikiendelea vyema Messi anatarajiwa kurejea katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Manchester City Octoba 19 maka huu.

No comments:

Post a Comment