Thursday, September 22, 2016

MOURINHO NA GUARDIOLA KUKUTANA TENA KOMBE LA LIGI.

MAHASIMU wa jiji la Manchester klabu za Manchester United na Manchester City zinatarajiwa kukwaana katika mzunguko wa nne wa michuano ya Kombe la Ligi, mchezo utakaopigwa kwenye Uwanja wa Old Trafford. United ilitinga hatua hiyo kwa kuitoa timu ya daraja la kwanza ya Northampton jana wakati City wao waliwatoa Swansea City kwa kuichapa mabao 2-1 na kupelekea timu hizo kukutana kwa mara ya pili msimu huu baada ya ile derby ya Septemba 10. Mechi zingine za hatua hiyo, West Ham United watakuwa wenyeji wa Chelsea, Tottenham Hotspurs wao watasafiri kuifuata Liverpool, Newcastle United watakwana na Preston huku Norwich City wakiivaa Leeds United. Wengine ni Hull City watakaocheza Bristol City, Southampton dhidi ya Sunderland na Arsenal wao watapambana na Reading. Mechi hizo zote zinatarajiwa kuchezwa wiki ya kuanzia Octoba 24 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment