Thursday, September 22, 2016

FALCAO BADO HALI TETE.

KOCHA wa AS Monaco, Leonardo Jardim amethibitisha Radamel Falcao bado ameendelea kubakia hospitali baada ya kupata mtikisiko wa ubongo katika mchezo wa Ligue 1 ambao walitandikwa mabao 4-0 na Nice. Falcao alianguka chini katika dakika za mwisho za kipindi cha kwanza baada ya kugongana vibaya na kipa wa Nice Yoan Cardinale na alikimbizwa hospitali kwa ajili ya vipimo zaidi. Jardim alimkosoa mwamuzi kwa kushindwa kutoa penati kwa mchezo mbaya ulioonyeshwa na Cardinale. Akihojiwa kuhusu hali ya Falcao, Jardim amesema bado yupo hospitali akiendelea kupatiwa matibabu kwa tukio lililomkuta jana. Jardim aliendelea kudai kuwa waamuzi wanapaswa kuyaangalia matukio hayo kwa ukaribu kwani anadhani kipa wa Nice alipaswa kupewa kadi nyekundu.

No comments:

Post a Comment