Thursday, September 22, 2016

RASMI: BUSQUETS ASAINI MITANO MIPYA.


KIUNGO wa Barcelona, Sergio Busquets amesaini rasmi mkataba mpya wa muda mrefu na klabu yake hiyo ya utotoni. Makubaliano kati ya pande zote mbili yaani klabu na mchezaji mwenyewe yalikuwa yameshaafikiwa toka Mei mwaka huu na kilichobakia kilikuwa ni kuwekeana na saini. Busquets sasa atabakia Barcelona mpaka 2021, huku kukiwa na kipengele cha kuongezewa miaka mingine miwili mpaka 2023. Taarifa hizo zimekuwa kama ahueni kwa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 28, ambaye alitolea mapema katika kipindi cha pili baada ya kuumia katika mchezo dhidi ya Atletico Madrid jana usiku.

No comments:

Post a Comment