Friday, September 23, 2016

BARCELONA INAWEZA KUSHINDA BILA MESSI - INIESTA.

KIUNGO wa Barcelona, Andres Iniesta amedai kuwa klabu hiyo inaweza kusonga mbele bila kuwepo nyota wao Lionel Messi. Messi alitolewa kufuatia kupata majeruhi ya nyonga katika mchezo wa Jumatano iliyopita dhidi ya Atletico Madrid ambao ulimalizika kwa sare ya bao 1-1 na sasa anategemewa kukaa nje kw akipindi cha wiki tatu. Pamoja na umuhimu wa Messi katika kikosi cha Barcelona, Iniesta amesema wanaweza kusonga mbele bila yeye kama wakiungana na kucheza kama timu. Iniesta aliendelea kudai kuwa anafahamu kuwa kikosi chao ni imara wakiwa na Messi lakini ni kiosi kizima ndicho kinachoshinda mataji hivyo ni matumaini yake wataendelea kucheza kwa umoja ili kupata matokeo. Mesi akiwa hayupo, Barcelona itakabiliwa na mechi tatu za ugenini ambazo ni dhidi ya Sportinh Gijon, Borussia Monchengladbach na Celta Vigo. Pia nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 anatarajiwa kukosa michezo ya kufuzu Kombe la Dunia ambapo Argentina itacheza dhid ya Peru na Paraguay Octoba 6 na 11 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment