Friday, September 16, 2016

NUSU FAINALI LIGI YA MABINGWA KUCHEZWA MWISHONI MWA WIKI HII.

MICHUANO ya Ligi ya Mabingwa Afrika inatarajiwa kuendelea tena mwishoni mwa wiki hii kwa mechi za hatua ya nusu fainali kuchezwa katika viwnaja tofauti. Kwa mara ya kwanza baada ya kupita miaka 15 michuano hiyo itashuhudia timu kutoka ukanda wa kusini mwa Afrika zikimenyana ambapo Zesco United ya Zambia itakwaana na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini. Afrika Kaskzini imekuwa ikitawala michuano hiyo huku timu za Misri, Tunisia, Morocco na Algeria zikishinda taji hilo mara 28 kati ya 51 huku Afrika ya kati wakilitwaa mara 12 na Afrika Magharibi mara 10. Kutokana na utawala huo wa Afrika Kaskazini sio jambo la kushangaza kuona mchezo mwingine wa nusu fainali ya michuano hiyo ukihusisha timu zao ambapo mabingwa mara tano Zamalek ya Misri watakwanaa na Wydad Casablanca ya Morocco ambao wamewahi kutwaa taji hilo mara moja. Mchezo huo wa mkondo wa kwanza unatarajiwa kuchezwa jijini Alexandria baadae leo huku ule wa Zesco na Sundowns ukitarajiwa kufanyika huko Ndola nchini Zambia kesho mchana.


No comments:

Post a Comment