Friday, September 30, 2016

ROONEY KUENDELEA KUWA NAHODHA WA UINGEREZA.

KOCHA wa muda wa timu ya taifa ya Uingereza, Gareth Bale amethibitisha kuwa Wayne Rooney ataendelea kuwa nahodha wa kikosi hicho. Southgate ambaye amechukua mikoba ya muda Jumanne hii kufuatia kuondoka kwa Sam Allardyce alizungumza na Rooney ambaye pia ndio nahodha wa Manchester United jana. Jumapili hii kocha huyo anatarajiwa kutaja kikosi chake ambacho kitajiandaa kwa ajili ya mechi za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia dhidi ya Malta na Slovenia. Mapema mwzi uliopita Allardyce alidai kuwa ni uamuzi rahisi kumuacha Rooney aendelee kuwa nahodha pamoja na kiwango kilichoonyeshwa na Uingereza katika michuano ya Ulaya mwaka huu.

No comments:

Post a Comment