Friday, September 30, 2016

LUKAKU ATAMANI KUWAFIKIA KINA SUAREZ.

MSHAMBULIAJI wa Everton, Romelu Lukaku anatambua bado anahitaji kuimarika kama anataka kufikia kiwango cha nyota wa Barcelona Luis Suarez na washambuliaji wengine wakubwa. Lukaku alifunga mabao 18 katika mechi 37 za Ligi Kuu msimu uliopita, lakini Everton hawakuwa na msimu mzuri hatua iliyopelekea kumaliza wakiwa katika nafasi ya 11, jambo ambali lilipelekea kutimuliwa kwa Roberto Martinez. Akihojiwa Lukaku amesema anahitaji mechi nyingi zaidi za kushinda ili kufikia kiwango cha mchezaji kama Suarez. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa kwasasa anafunga mabao kama wao lakini anahitaji kutengeneza mabao kama wafanyavyo kina Sergio Aguero, Suarez, Karim Benzema, Roberto Lewandowski na wengineo.

No comments:

Post a Comment