Friday, September 30, 2016

WENGER AACHA MILANGO WAZI YA KWENDA KUINOA UINGEREZA.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema yuko tayari kuja kuinoa timu ya taifa ya Uingereza siku za usoni, lakini kwasasa mkazo wake uko katika klabu yake hiyo. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo, Wenger amesema siku moja kama atakuwa hana kazi anaweza kukubali kuinoa nchi hiyo. Meneja huyo raia wa Ufaransa atasheherekea miaka 20 ya kuwa na Arsenal Octoba mosi mwaka huu na mkataba wake unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu. Chama cha Soka cha Uingereza-FA kwasasa kinatafuta meneja mpya kufuatia kuondoka kwa Sam Allardyce Jumanne iliyopita.

No comments:

Post a Comment