Friday, September 30, 2016

CONTE KUPEWA FUNGU JANUARI.

MMILIKI wa Chelsea, Roman Abramovic yuko tayari kumsaidia Antonio Conte baada ya kumwambia Muitaliano huyo kuwa ataruhusiwa kufanya usajili wa wachezaji kadhaa katika kipindi cha usajili wa Januari. Mkutano baina yao unatajwa kufanyika katika uwanja wa wa mazoezi wa Cobham wiki hii ambapo Conte aliwasilisha mapendekezo yake kwa mmiliki huyo akidai kupewa ruhusa ya kusajili. Taarifa kutoka ndani zinadai kuwa Abramovic anadhani Conte alirithi kikosi kilichopitwa na wakati ambacho kilitwaa taji la Ligi Kuu miaka miwili iliyopita lakini amefurahishwa kwa jinsi alivyokisuka na kukirejeshea makali yake. Conte anataka kukijenga upya kikosi hicho na imefahamika kuwa atapewa ushirikiano wowote ikiwemo wa kifedha na mmiliki huo.

No comments:

Post a Comment