Friday, September 30, 2016

KLOPP ATANGAZA KUSTAAFU UKOCHA KABLA YA KUFIKISHA MIAKA 60.

MENEJA wa Liverpool, Jurgen Klopp tayari ameshaanza kufikiria kuhusu maisha baada ya soka na ameweka wazi amepanga kustaafu kabla ya kufikisha miaka 60. Meneja huyo mwenye umri wa miaka 49, alianza shughuli hizo katika klabu ya Mainz mwaka 2001 na pia kufanya kazi kwa mafanikio Borussia Dortmund kabla ya kutua Liverpool mwaka 2015. Klopp anafurahia maisha ya Anfield lakini amekiri haoni kama ataweza kuendelea na kazi zaidi ya kipindi cha miaka 10 ijayo. Akihojiwa Klopp amesema anafahamu itakuja siku ya kuamua kwamba kazi hiyo inatosha na kuna uwezekano mdogo sana wa kuendelea na kazi hiyo akiwa amefikisha umri wa miaka 60. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa atarejea zake nyumbani Ujerumani kwenda kuishi huko lakini hadhani kama atarudi akiwa kocha.

No comments:

Post a Comment